Читать онлайн книгу «Sayari Saba» автора Massimo Longo

Sayari Saba
Massimo Longo E Maria Grazia Gullo
Sayari Saba: kwenye mfumo sambamba wa jua, watu kutoka sayari saba tofauti wanajihusisha katika mapambano ya wakati ambayo yataamua hali yao ya baadaye. Hatima ya wahusika wakuu imeingiliwa na, chuki,mapenzi na tamaa, katika jaribio la kutawala au kukomboa watu wa mfumo wa jua wa KIC. Sayari za kubuni na za kipekee, jamii tofauti na tamaduni zao zitajumuika kwenye vituko vya ajabu ili kupigana dhidi ya tamaa ya mamlaka ya adui mcheshi


Maria Grazia Gullo - Massimo Longo

SAYARI SABA

Mifupa ya nje na kitu cha Parius

Imetafsiriwa na Kennedy Cheruyot Langat
Hakimiliki © 2019 MG Gullo - M. Longo
Picha ya Jalada na michoro imeundwa na kuhaiririwa na Massimo Longo
Haki zote zimehifadhiwa
YALIYOMO


Sura ya Kwanza

Bahari ya Ukimya

Jenarali Ruegra alikuwa akitazama angani kupitia shimo kubwa kwenye dirisha ndogo kwenye dambra. Ilivutia kuona mfumo mzima wa sayari wa KIC 8462852 na sayari zake saba kwenye obiti. Wakati huo, angeweza kuona tu sayari tano kati ya hizo: Sayari ya Carimea, ambayo ni nyumbani kwake, ilikuwa na anga ya kijivu, ambayo ilimaanisha ilikuwa imepangiwa nafasi ya uongozi; Medusa ilikuwa ya bluu na ya kupendeza, ambayo ilikuwa na sumaku na hatari kama wakaazi wake; Oria, ambayo ilikuwa ndogo na tasa kama mwezi, na pia ilikuwa nyeupe kutokana na akisi ya mwangaza wa Jua letu. Umbali usio mrefu kutoka Oria, kulikuwa na Sayari ya sita ambayo ilikuwa kijani kibichi, na ambayo ilikuwa na ujamii zaidi na ilikuwa imeendelea kiteknolojia miongoni mwa sayari nyingine; na Eumenide, iliyokuwa na anga ya waridi, ambayo ilikuwa ya kuvutia sawa na wakaazi wake wa kutisha.
Yote hayo hivi karibuni yatakuwa mali ya watu wa Aniki na yeye atateuliwa kiongozi mkuu. Alihitajika kuwa mvumilivu na kukamilisha mpango wake: huku akiwa na Ngozi iliyo na sheria mikononi mwake kila kitu na kila mtu atafanya kulingana na mapenzi yake.
Jenerali Ruegra alikuwa akitazama angani kupitia dirisha ndogo kwenye dambra lake na angehisi tamaa ya uongozi ikikua ndani yake. Ilikuwa mwaka wa 7692 tangu kuanzishwa kwa utawala wa Aniki. Ruegra aliamshwa ghafula kutoka kwenye ndoto ya adhama. Chombo chake cha angani kilikuwa kimegonga kitu: walikuwa wanavuka mviringo wa Bonobo. Ingekuwa bora kuelekea kwenye dambra ya kuthibiti chombo. Ingawa kutua kwenye sayari hiyo ilikuwa utaratibu wa kawaida, bado inaweza kuwa na matatizo kadhaa.
Punde tu alipoingia katika dambra ya kuthibiti chombo, alilakiwa kwa heshima na wasaidizi wake.
Utaratibu haukuwa unaenda vizuri kama ilivyopangwa awali: kuna kitu kilikuwa kimegonga meli hiyo ya angani, kama alivyohofia.
"Jenerali, eneo la 8 limeharibiwa. Jiwe limetugonga. " Nahodha akaripoti mara moja.
"Tenga eneo hilo mara moja na uendelee kuliondoa sehemu hiyo."
Nahodha aliamuru mchakato wa uokoaji katika eneo lililotengwa:
"Uokoaji wa haraka katika eneo hilo ...
Ulitenge! Usipoteze wakati wowote! " "
Afisa huyo mara moja alitekeleza amri hiyo. Hakuna aliyethubutu kumfanya Ruegra aone kuwa hatua hiyo itachukua maisha ya wanajeshi wengi bure.
Kuta nyingi zilizokuwa zikitenganisha eneo hilo kutoka kwa sehemu nyingine za meli hiyo ya angani zilifungwa. Wanajeshi wachache tu ndio walioweza kuruka kwa haraka chini ya mlango uliotenganisha eneo hilo na nyingine ili kuepuka kusombwa. Kwa bahati mbaya, walishuhudia wenzao, ambao walikuwa wameishi pamoja hadi dakika chache zilizopita, wakipoteza matumaini walipogonga kuta hizo na kisha wakatoweka.
Utengaji wa eneo lililoharibika ulikamilishwa, na eneo hilo likaachwa.
Vyombo vyote vya angani vya Carimea vilikuwa vya angani na vilikuwa na umbo la mdudu mkubwa wa trilobiti. Vilikuwa vimegawanya kwa vipande vipande ili eneo fulani liondolewe kwa haraka linapoharibika. Kwa njia hii, wafanyikazi wataafikia matokeo mazuri wakati wa vita. Sehemu zote mbili za katikati na mkia, ambazo zilikuwa na umbo la ganda la chaza, zinaweza kuondolewa. Dambra ya kuthibiti chombo hicho, inayoshirikisha sahani kubwa na sura ya nusu mviringo ambayo inakuwa na pembe nyingi katika sehemu nyingine na kuwa ‘mgongo’ wa chombo hicho, haiwezi kuondolewa.
Zilikuwa zimezungukwa na mnyoosho usio na mwisho zilizoundwa na miviringo kubwa ya kijivu ambayo ilikuwa imezunguka sayari ya Bonobo. Miviringo hiyo ilikuwa inajumuisha vifusi vikubwa vilivyosababishwa na kifo cha kimondo ambacho kilikuwa kimesonga karibu na KIC 8462852.
Bonobo, ambayo ni sayari ya pili iliyo mbali kutoka kibete, pia ilijumuisha donge ambalo lilikuwa limekusanya vifusi vingi. Kwa njia hii, ilikuwa imeacha sayari ndogo ya Enas na ilikuwa imeunda mandhari ya kiajabu katika galaksi yote.
Sayari hiyo ilipatikana katikati ya miviringo hiyo. Ilikuwa ina mali nyingi sana na tofauti hivi kwamba ilitumika kama hifadhi ya kifalme ya Aniki ya uwindaji, watumwa na vifaa. Watu wake ambao walikuwa kama binadamu walikuwa wamekwama katika mwanzo wa utawala wao. Watu wa Bonobo walitembea wima, walikuwa na miguu ya yenye viungo vya kushika na miili yao ilikuwa na manyoya.
Walikuwa kubwa kama masokwe lakini hawakuwa werevu na walikaa kama watoto. Wangezaa haraka na walikuwa na nguvu, ambayo ingawafanya wakimilifu.
Bonobo ilikuwa sayari ya pekee ambayo ilitwaliwa na wana-Aniki ambayo ilisalia chini ya utawala wao. Na ni kwa sababu tu sayari hizo mbili zilikuwa zinafanana na zilikuwa zinazunguka KIC 8462852.
Carimea ilikuwa imeweza kutwaa utawala wa sayari nyingine pia, lakini kila mara walikuwa wanapoteza uthibiti kutokana na uasi uliochochewa na muungano wa sayari hizo nne, ambazo lengo lao lilirahisishwa na kuwa karibu kwa mzingo.
Meli ya angani kilitua kwa wakati ufaao. Katika makao makuu, vifaa tayari vilikuwa vimetayarishwa kwa mgao. Ruegra alishuka chini ili kuongea tu na Mastigo, Gavana wa eneo hilo. Jenerali huyo hakumpenda huyo mtu wa Evic hasa, lakini uongozi wake kwa wakaazi ulikuwa na ufanisi. Alikuwa wa kabila maarufu huko Carimea.
Wa-Eviki walikuwa wakubwa, reptilia wa kijani-kijivu ambao wangetembea kwa miguu yake ya nyuma iliyokuwa minene na yenye nguvu. Walikuwa wadogo kidogo kuliko wa-aniki isipokuwa nyuso zao, ambazo zilifunikwa kabisa na magamba. Nyuzo zao ambazo nusu zilikuwa na umbo la duaradufu zingenyooka nje kutoka maskio na kuchukua umbo la nusu kengele. Hawakuwa na mashavu yoyote na mapua yao yaliyokuwa kama nyoka na hayakuonekana kabisa. Walikuwa wakali, lakini hawakuwa werevu hasa, walikuwa kabila pekee ambalo lingengangania mamlaka na Wa-aniki kwa idadi na nguvu. Walivaa koti refu la kiuno la hariri ambalo linafunikwa na miguu yao na ambayo inafungwa kwa vifungo kwenye kifua. Ili kupata usaidizi wao, Ruegra alikuwa amemteua mmoja wao kuwa Gavana wa Bonobo.
Jenarali alikaribishwa kwa utukufu kwenye ukumbi wa glasi kwenye jengo la serikali, ambako kuna mazingira mazuri ya kitropiki ya kupendeza. Ulikuwa usiku wa kustaajabisha na anga ilikuwa imewashwa kwa akisi wa miviringo hiyo.

Ruegra alikuwa akitazama kupitia glasi iliyokuwa ikiakisi picha yake.
Rangi ya mwili wake thabiti, iliyokuwa imefunikwa na ngozi kavu, ambazo zingebadilisha rangi kulingana na mazingira. Sura haikuweza kutambulika kati ya miti iliyo nje. Taji ngumu iliyotengenezwa kwa tishu za karatini na ilikuwa na urefu wa Kudus 30 au inchi 11 ilikuwa imepamba sura yake, kuanzia kichwa. Taji hiyo ingefunguka kama kuna hatari na inakuwa silaha ambayo Wa-Aniki walitumia wakati wa mwanzo wa utawala wake kumtisha adui. Inapofunguliwa kwenye mkono, ingetumika kama ngao.
Kutokana na uso wake wa mviringo ngozi kavu zingesinyaa na kuwa sawa kwa rangi. Chini ya paja la uso wake, nyusi na kobe zake za bluu za karatini hufanya macho yake kubwa ya kijani kibichi na mashavu yake laini yenye rangi yaliyodhihirika. Pua lake kubwa lililolemaa, kama la bondia, lilihitiliafiana na sura yake. Mdomo wake uliwiana vizuri: mdomo wake wa kijani ulikuwa kubwa na nono.
Waaniki walikuwa wakubwa zaidi kwa urefu miongoni mwa watu wote katika mfumo wa jua na sayari zake na kwa sababu hiyo daima wamekuwa juu katika piramidi ya Wanyama wawindaji.
Sawa na Wa-aniki, Ruegra kwa kawaida huvaa sketi iliyona vipande viwili vilivyopasuliwa ambavyo vingeonesha Ngozi kavu kwenye mwilini wake. Begani angevaa rasi, ambayo inadhamiriwa kuonesha tabaka na majukumu yake. Rasi yake ilikuwa na rangi ya dhahabu, ilioashiria cheo chake cha amri na ilipambwa na sura ya rangi ya moshi-kijivu na nakshi ya rangi sawa ilioonesha ndege ya uwindaji wa Atrex.
"Ninasalimu asiyeweza kushindwa miongoni mwa watu wa Carimea. Unakaribishwa kila wakati katika nchi yetu, jenarali wangu. Safari ilikuwaje?" akamsalimu Mastigo kwa kumwinamia kidogo.
"Ilikuwa nzuri. Ujumbe unaendelea kwa njia nzuri." Ruegra akadanganya. "Nahitaji tu kupumzika. Pete hizo za sayari hufanya meli ya angani kutetemeka kidogo." Alisema ili aachane na mzungumzaji.
Mastigo alimpa kinywaji cha matunda ya huko ili aburudike baada ya safari ndefu baina ya sayari. Ilikuwa afadhali kwa Jenerali kuketi kwani alihitajika kuripoti tukio lisilo la kawaida.
"Ninatukio lisilo la kawaida ambalo linahitaji kuwasilishwa kwako. "Siku mbili zilizopita za Bonobo, tuliona chombo cha angani cha biashara kilipokuwa kikiingia eneo letu bila ruhusa. Walinzi hawakuweza kuisimamisha kwa wakati ufaao. Kwa hivyo, ilitumbukia katika Bahari ya Unyamavu kabla hatujatathmini hatari zake halisi.
Tumefanya utafiti na tumepata kwamba mmiliki amekiuza kwa mwanamke mmoja wa Eumenide. Nimetuma askari kadhaa wa doria kuchunguza eneo linalodaiwa kutua. Lakini kama unavyojua, haiwezekani kupokea mawasiliano ya aina yoyote kutoka Bahari ya Unyamavu. Kwa hiyo, tunachotakiwa kufanya ni kusubiri."
Ruegra alikasirishwa na jinsi Gavana alivyoshikilia ukweli huo usio na maana na akauliza:
"Ni nini cha ajabu kuhusu hayo? Sielewi..."
"Angalia mahali ilikuwa inaelekea..." akasema Mastigo akionesha ramani ya Bahari ya Unyamavu.
"Hapa ndiko mahali ngome takatifu ya Bonobo inapopatikana..." Ruegra akanong’oneza.
"Ndio sababu nilichukua huru wa kuripoti tukio dogo kama hilo. Nimetuma timu kuchunguza eneo hilo. Inaweza kuwa ililingana tu, lakini ni heri kuwa salama kuliko kusema pole. Mahali hapo pamejaa miujiza. Ingekuwa makao makuu mazuri kuanzia migogoro, ukizingatia ukosefu wa mawasiliano na ishara za rada. Ni kama shimo jeusi.
"Unaweza kuwa sahihi. Endelea kunisasisha, Mastigo. Sasa ni bora ikiwa nitapumzika. Kesho tutaondoka alfajiri."

Usiku huo Ruegra alikuwa na vitu vingine vya kufikiria. Baada ya kurudi chumbani kwake, aliketi kwenye sofa laini na kujipatia kinywaji aina ya Sidibé, pombe kali ya kienyeji inayopatikana kwa cacti. Alikuwa akitazama angani huku fikra zake zikikimbizana kama mawimbi kabla ya dhoruba.
Safari ambayo alikuwa tu amemaliza imekuwa ya janga kabisa, kinyume na kile alichokuwa amemwambia mshirika wake anayemwamini.
Alikuwa amezuru Mwezi wa sayari ya Enas, haswa kwa koloni ya uchimbaji madini ya Stoneblack, kambi ndogo inayofahamika sana kwa marumaru yake. Jenarali huyo alikuwa akihitajika kukutana na mtu ambaye babaye mwenyewe alikuwa anamheshimu sana: adui wa zamani wa Carimea.
Koloni hiyo ilitawaliwa na kabila la Triki. Walikuwa watu kutoka Carimea, kama Wa-aniki, lakini walikuwa na ushawishi wa pili kwenye usimamizi wa sayari hiyo.
Walikuwa wamejitolea kuhudumu, lakini hawaaminiki. Walikuwa wamejidhihirisha kuwa wasaliti mara tu upepo unapobadilisha mwelekeo. Hata rafiki zake mwenyewe wangeweza kupanga njama dhidi yake kwenye Mwezi huo. Kwa hivyo, ilibidi kufanya ukaguzi huo uonekane kama ziara ya ghafula akiwa na nia ya kurudisha baadhi ya visukuu vya mwezi kwa nduguye wakati wa kurudi.
Ruegra alitembea mbele ya maafisa hao. Alileta kiwiko chake karibu na bega lake na huku mkono wake ukiwa sambamba na sakafu na karibu na kinywa chake, akawasalimia. Ishara hiyo ilionesha ukimya mbele ya amri yake pamoja na utii kamili. Walikuwa bado wamenyamaza mbele yake.
Koloni hiyo ya uchimbaji madini iliajiriwa kama wahalifu wanaofanya kazi ya lazima na wafungwa wa kivita kufanya kazi kwa gharama rahisi. Walinzi hao wangemlinda mtumwa mmoja hasa...Alikuwa mtu wa Ruegra. Sio tu kwamba alikuwa mtumwa wa kiwango cha juu, lakini pia alikuwa amepata heshima kutoka kwa watumwa wenzake na aliweza kuwaakilisha.
Jenarali huyo, aliyeandamana na nahodha na kufuatiwa na wanajeshi, aliwekwa kwenye chumba cha kupumzika na cha kutolea amri, amchacho kilikuwa kimetengewa afisa huyo.
Nahodha huyo alitoa heshima zake na kuuliza iwapo angetaka kitu.
Ruegra hakupoteza wakati wowote. Alikataa ofa hiyo na akaamuru:
"Ninataka kuthibitisha hali ya wafungwa wa kisiasa ambao walichukuliwa wakati wa vita dhidi ya Sayari ya Sita. Wacha niongee na afisa mwenye cheo cha juu."
"Jenarali Wof?"
"Ndio, haswa. Mlete kwangu. " "
"Ndio, bwana."
Kamanda akaguna kwa walinzi na dakika chache baadaye walirudi chumbani akiandamana na mtu wa makamo. Alionekana mchovu na kukosa nguvu, lakini bado alikuwa na kiburi na sura ya mpiganaji asiye na hofu.
"Tuacheni." akamrishwa Ruegra.
Alisalia pekee akiwa na adui mwenye akili kali. Alikumbuka kuwa wakati wa vita alikuwa ameweza kubadilisha hali mbaya ambayo ilikuwa imetabiri kifo chake, shukran kwa kufikiria kimkakati na licha ya kuwa na watu wachache kutoka Sayari ya sita chini ya utawala wake.
Alisita kwa sekunde kadhaa kabla ya kuzungumza. Alikuwa tayari amewaza kuhusu mikakati kadhaa wakati wa safari yake. Alijua kwamba haingewezekana kumshika adui yake bila kufahamu. Ilikuwa wakati wa kuchukua mmoja na kuanza makabiliano.
Aliamua kuendelea na ibada hiyo ya kumsifu akitarajia kwamba uzee wake na uchovu wake umemfanya kudhoofika zaidi.
"Nakusalimu, Wof. Ninaweza kusema kwamba hauonekani vibaya licha ya kutopewa matibabu bora. Hata hivyo nimeamrisha upatiwe vitabu na elimu. " "
"Muda mrefu sijakuona." alisema Wof, akimtazama jenarali huyo na macho yake ya kina na meusi. "Ni nini kilikuleta mahali hapa ambako imesahaulika na mwangaza, ambako giza inatawala?"
"Nilikuja hapa kuongea nawe kuhusu baba yangu. Nakumbuka kuwa nikiwa mtoto angefikria kuhusu Ngozi ambayo ulijua siri zote kuihusu. Sasa kwa kuwa ninazeeka, wakati mwingine ninafikiria kumhusu na kushangaa iwapo kuna ukweli kuhusu hadithi hiyo."
Wof alijaribu kuficha ushangao wake kwa kupapasa nywele zake hizo ambazo zilikuwa zinampa sura uso wake nyeusi.
"Baba yako alikuwa akisema ukweli, lakini inavyoonekana, hakufikiria kwamba ulikuwa mwaminifu wa kutosha kujua maelezo yote.
Pia alijua siri zote ambazo hazijazungumziwa. Ruegra alishangaa. Baba yake alikuwa ametaja siri hiyo mara nyingi, lakini hakuwahi kuwa na hamu ya kufichua.
"Nini mbaya, Jenerali? Unashangaa kwanini hakukuambia zaidi kuihusu?"
"Labda umri wangu mdogo na msukumo wangu ulinifanya msikilizaji mbaya."
"Afadhali niseme kwamba tabia yako ni hamu ya kuwa na mamlaka na utawala wa kijeshi."
"Mamlaka ni muhimu kudumisha utulivu na uimara." Akasisitiza Jenarali huyo, baada ya kusimama akiwa amekasirika.
"Una imani na utaratibu, ukiwa umeajiriwa kuhudumia mtu mmoja na kwa utulivu wa kabila moja." akajibu Wof.
Ruegra alianza kutembea kwa uwoga. Alikuwa tayari amepoteza uvumilivu wake, lakini alijua vizuri kuwa hakuna mateso au ulafi ambao ungefanya kazi kwa mtu ambaye alikuwa ameketi mbele yake. Tumaini lake la pekee lilikuwa kupata uaminifu wa mtu huyo.
Alianza kuwa mjanja na kudanganya:
"Unajua, kwa kweli ninamheshimu baba yangu. Wakati nilipokuwa mdogo ulikuwa ukisema kwamba ninafanana naye... Wakati huo, nilikuona kama bwana...."
"Nini inakufanya kufikiria kwamba nitafichua jinsi ya kupata ngozi hiyo? Usafi huo uliokuwa nao utotoni ulipotea haraka, Ruegra, na nia ya kujithibitisha ilichukuliwa na kiu ya mamlaka."
"Mimi si Aniki ambaye unamkumbuka wakati wa vita. Nitajua kuthibiti mamlaka kwa usawa. Baba yangu alifanya makosa kwa kukosa kuniambia kila kitu." "Jenerali alisema kwa hasira nyingi.
"Ikiwa ilibidi uje kwangu, inamaanisha kuwa haukustahili kuaminiwa na baba yako. Ni baba wa aina gani anayeficha maarifa kutoka kwa mwanawe? Kuna taabu katika ishara zake. Nani aliyebora kuliko yeye alikujua na mimi ni nani kufichua kila kitu kwako na kupuuza kabisa tathmini yake? Kama unavyoona siwezi fanya chochote lakini kuheshimu nia yake na kuheshimu kumbukumbu yake." Alisema Wof. Kisha alisimama na kusema kwaheri kwa mnyongaji wake.
Tukio hilo halingeondoka katika akili ya Jenarali, ambaye aliendelea kutazama angani akiwa na glasi mkononi kwenye usiku huo wa Bonobo uliokuwa joto.

Asubuhi iliyofuata, Ruegra alichunguza binafsi kazi ambayo ilikuwa imekamilishwa kubadilisha sehemu iliyoharibika ya chombo cha angani.
Mastigo alikuwa amefuatilia vizuri na mafundi wake walikuwa wamefanya kazi nzuri kama kawaida. Wakaondoka kwa wakati uliowekwa na kurejea nyumbani.

Siku zilikuwa zikipita na Ruegra alikuwa na haraka ya kurudi nyumbani. Aliogopa njama, ingawa kakaye, ambaye alikuwa akiongoza wakati hakuwepo, atampa Jenarali ripoti za kila mara kuhusu hali hiyo. Hapakuwa na kitu cha kuwa na wasi wasi nacho. Carimea ilikuwa mchanganyiko wa jamii. Makabila tofauti walikuwa wakipigania utawala dhidi ya Wa-aniki, lakini Wa-aniki walikuwa wamewaondoa idadi inayodhihirika ya wapinzani wakati wa utawala wao. Ilikuwa imeanzishwa na vikundi kadhaa vya mfumo tofauti wa jua, wengi wao walikuwa watalii, watafutaji wa bahati au wafungwa wa awali ambao walikuwa wakitafuta ardhi kuanzisha maisha yao upya. Sehemu ndogo tu kati yao walitoka kwenye sayari hiyo. Kwa kweli, watu wa sehemu hiyo walikuwa wametawaliwa kishenzi na kutengwa.
Njiani wakirudi, huku akiwa ameketi katika kiti cha kuthibiti chombo kwenye dashibodi, Ruegra alikuwa akifikiria kuhusu maneno ya Wof. Kwamba "Baba yangu alijua" iliendelea kusikika akilini mwake.
Kisha kwa ghafula, akafikiria nyakati zote baba yake angeondoka wakati wa msimu wa uwindaji na kabla ya vita vyote. Mahali alipenda kwenda ilikuwa kwa kweli ardhi ya Bonobo, haswa kwa Bahari ya Unyamavu.
Wakati fikra hizo zilikuwa zikitembea kwenye akili yake, alipata utambuzi wa kuangaza na kufikira:" Mbona sijafikiria kuhusu haya awali?" Kitu au mtu huku huenda alimpa taarifa zaidi kuhusu ngozi hiyo iliyo na siri.
Alihusisha uhisi wake na ripoti ya Mastigo kuhusu chombo cha angani cha kibiashara. Labda mtu alikuwa mbele yake.
Aliamuru kubadilisha njia mara moja. Walikuwa wanarejea huko Bonobo.

Mastigo, aliyekuwa ameshangaa baada ya kuwaona wakirudi, alikimbia kuelekea chombo hicho cha angani.
"Ninasalimu mtu ambaye hawezi kushindwa miongoni mwa watu wa Carimea. Jenerali, mbona umerudi?"
"Nimetafakari kuhusu kutua kwa chombo hicho cha angani, na imenishawishi kurudi na kushughulikia binafsi hali hiyo."
"Kwa mara nyingine, umefanya jambo la busara. Wataarifu wangu hawakurejea Bonobo. Kwa hivyo, niliamua kuzuru eneo hili mimi binafsi. Niligundua kuwa walikuwa wameondolewa na watu wasiojulikana."
Ruegra alikuwa akitumaini kuwa Gavana wake hajaharibu uwezekano wote wa kupata taarifa kwa kuwa alijua njia zake.
"Hakuna kilichoachwa huko." akaripoti Mastigo mara moja, ambaye alikuwa akionekana kuridhika kama mtoto ambaye alitesa mawindo yake madogo.
Ruegra alijizuia kumshambulia msemaji wake na kumwuliza mahali wafanyakazi wake walikuwa wameenda.
Mastigo alichukua pumzi mzito, akifahamu kuwa haitakuwa Habari njema.
"Hatukuweza kuipata. Lazima wamekimbia."
"Sio tu uliharibu ushahidi wote, lakini pia uliwaacha wafanyakazi kutoroka! Ulikuwa huna ujuzi wewe! Nipeleke huko!"
Kisha, baada ya kufikiria tena alitambua kuwa haitakuwa wazo nzuri kumruhusu Mastigo kufahamu kuhusu mipango yake.
"Niandalie wafanyakazi. Nitaondoka kesho bila wewe."
Sura ya Pili

Upanga wa jiwe ulikuwa ukining'inia juu ya vichwa vyao.

"Tujiandae? Huenda tusikaribishwe tukapowasili! "alishangaa Oalif, ambaye ni mwerevu zaidi kwenye kundi hilo.
Wafanyikazi walijumuisha wanachama wanne kutoka sayari ambazo zilikuwa zikipambana dhidi ya utawala wa Carimea. Walichaguliwa kwa sababu ya historia yao ya matumizi na pia uwezo wao wa mwili na akili. Kwa pamoja wangeunda timu ambayo ingeweza kufanya kazi yoyote, nyingi na kimkakati. Wajibu wao ulikuwa kuhakikisha amani na sio tu hatua za kijeshi, lakini pia shughuli zinazohusiana na ujasusi na uratibu kati ya watu tofauti.
Baraza la Muungano wa Sayari Nne lilikuwa limewateua kuwa "Tetramiri", ambayo ilimaanisha kwamba wanaweza kufaidika na Serikali kutoka kwa mamlaka maalum na kazi hadi kukamilika kwa utume wao.
Meli ndogo cha angani cha kibiashara kilikuwa kikivuka miviringo mikubwa za kijivu za Bonobo na kilikuwa kikiendelea kuelekea Bahari ya Ukimya.
Aina hiyo ya chombo cha angani ilitengenezwa kwa minajili ya usafirishaji wa bidhaa. Iliumbwa kama mabomba sambamba yaliyo na kingo zilizobutu mbele ili kutoa mwendo mzuri angani. Juu ya hayo, ilikuwa wameweka mabawa madogo, yanayoweza kutolewa ambayo yalitumika wakati wa kuvuka anga. Nyuma, kulikuwa na mlango mkubwa wa kushikilia ambao ungefunguliwa katika sehemu tatu kama taji ya maua na ilitumika wakati wa kupakia na kupakua. Vyombo hivyo vya angani vilikuwa kubwa na mwendo wa polepole. Vingeondoka na kutua sambamba na ardhi bila hata kuacha nafasi yoyote ya badiliko la mwelekeo wa mapigo, kama vyombo vingine vile vya angani.
"Jitangaze." sauti ya metali ilitoka redioni.
"Sisi ni wafanyabiashara, bwana." alijibu Oalif.
"Tunaweza kuona. Lakini ni nani na ni nini mmebeba? Una leseni? "
"Settimo kutoka Oria, bwana."
"Nambari ya leseni, sasa!" alisisitiza mlinzi.
"34876."
"Wewe haumo katika orodha yetu. Badilisha njia mara moja. Huna ruhusa yoyote ya kutua katika eneo hili. "
"Mawimbi ni dhaifu, bwana. Sikusikii. Leseni namba 34876. "alisema Oalif kwa mara ya pili, akijifanya hasikii kile mlinzi alikuwa anasema.
"Ruhusa ya kutua imekataliwa!"
"Hatuwezi kunakili wewe, bwana." alisisitiza mtu huyo wa Bonobo kisha akawaambia wafanyakazi wake akisema: "Tuko ndani, jamani! Tunavuka ukungu katika Bahari ya Ukimya! "
Oalif alikuwa rubani mzoefu, na akiwa Bonobo, alikuwa mjuzi wa kiwango cha juu wa sayari yake ya asili. Walakini, hakuendana na tabia rahisi na nyepesi ambazo kawaida zilipewa kabila hilo. Kabila lake lilikuwa halijawahi kutolewa kwa Waaniki, na kwa sababu hiyo lilikuwa limelipa bei kubwa. Wakati wa vita vya mwisho, baada ya kupoteza udhibiti wa sayari yao wenyewe, walikuwa wamehamishwa na kushikiliwa na Muungano wa sayari, ambao walikuwa wakipanga maandamano ya ndani. Lengo lao lilikuwa kupata tena udhibiti wa sayari.
Mwili wa Oalif ulikuwa na nywele nyeusi za mwili ambazo hazingeonyesha ngozi yake nzuri. Eneo tu linalozunguka macho yake ya kijani na mashavu yake hayakuwa na nywele. Alikuwa na ndevu nene, zilizochongoka, ndefu hadi kifuani, na angeweka nywele zake ndefu kama mkia wa farasi nyuma ya shingo lake.
Oalif alikuwa mtu anayefaa kwa utume huo, lakini kwa bahati mbaya, angelazimika kukaa ndani ili asije akaonekana. Kwa kweli, alikuwa akitafutwa: uso wake ulijulikana sana, na hawakujua watakutana na nani au nini.
Meli ya angani ilitua katika eneo la kijani kibichi, lenye jua lililovukwa na mto mpana na maji ya kina kirefu na safi ambayo yangeonyesha sakafu ya mto. Mwisho huo ulifunikwa na aina mbali mbali ya mawe, kama vile kwenye picha ya mtaalam wa maoni.
"Njia bora ya kuficha kitu, ni kufanya hivyo hadharani. Oalif, washa mtambo wa kuficha mara tu tunaposhuka. Asante, umekuwa mzuri. "Alimpongeza Ulica, wa Eumenide.
"Mahali hapa ni pa ajabu. Mara tu unapoingia ndani, ukungu unaozunguka hupotea na miale ya KIC 8462852 huanza kutia joto angani kana kwamba ilikuwa majira ya joto. "Aligundua Zàira kutoka Oria mara tu alipotua.
"Harakisha. Tuna muda mdogo wa kupata makao kabla ya jioni. Mastigo hatatuachia wakati mwingi wa kutafuta nyumba ya monasteri "aliamuru Xam kutoka Sayari ya Sita, ambaye alikuwa mshiriki wa nne wa kikundi hicho.
"Wacha tufuate mkondo wa mto." alipendekeza Zàira. " Msitu unaouzunguka utatufunika wakati tunachagua njia inayofaa zaidi. "
Walijitosa msituni. Xam na Zàira walikuwa wakiongoza njia wakati Ulica alikuwa akitafuta njia sahihi ili kufikia kijiji cha Bonobo. Huko walikuwa wanapanga kupumzika na kupata habari zaidi kuhusu monasteri ya Nativ, lengo lao kuu.
Xam, shujaa kutoka Sayari ya Sita, alikuwa mwanadamu ambaye alikuwa amesimama wakati wa vita kwa ujasiri wake na ubinadamu.
Alikuwa kijana mrefu, mwenye misuli. Alikuwa na ngozi nzuri na nywele fupi nyeusi, zilizokunjika. Midomo yake kamili ilikuwa imefichwa na ndevu nene zilizonyooka. Juu ya suruali yake nyembamba, alikuwa amevaa mkanda wa teknolojia wa kazi nyingi ambao ulibuniwa na watu wake ili kupata hali bora maishani au kifo. Pande nyingine ya mwili wake ilifunikwa na jeli iliyotumiwa na watu wa Sayari ya sita kudumisha hali ya joto ya mwili katika hali yoyote ya hali ya hewa.
Zàira, ambaye alikuwa rika lake, alitoka Oria, sayari yenye anga finyu. Silaha nyeusi, ya asili ilifunikwa mwili wake, kuanzia juu ya paji la uso wake na kunyooka nyuma hadi mkia wake: ilikuwa tabia ya kabila hilo. Sufi fupi na nene ilifunikwa mwili wake wote, isipokuwa uso wake kama wa kibinadamu ambao macho mawili ya kijani kibichi yenye kupendeza yalisimama. Kwenye paji la uso wake, kwa pande za silaha alikuwa na vifungu viwili ndefu vya nywele nyeupe ambazo kwa kawaida angefunga kwa kusuka hadi mabegani.
Ulica, mdogo kati ya hao wanne, alikuwa mwanasayansi ya kiwango cha juu na mtaalam wa hesabu kutoka Eumenide. Alikuwa wa tabaka wa juu na wa kifahari kama kipepeo. Mwili wake ulikuwa umefunikwa kwa johari ya uwazi pazia la asili ambayo ilionekana kama mabawa ya kipepeo.
Kwa kufungua mikono yake, mabawa yake yangeenea wazi na kumruhusu aruke. Yalikuwa yamekunjwa na kushushwa chini nyuma ya mikono yake. Yalionekana kama tatoo ya henna: vipande nyembamba, vya hariri ambavyo vingeweza kunyoosha na kutumiwa kama lasso au mjeledi.
Jaribio hilo lilidumu kwa muda mrefu kuliko kawaida kwa sababu ya hitilafu kwenye kifaa cha ufuatiliaji iliyosababishwa na athari nyingine ambazo zilikuwa zikitokea katika vifaa kwenye Bahari ya Ukimya. Tukio hilo lisilotarajiwa liliwafanya waachane na njia sahihi kando ya ziwa na kusababisha ucheleweshaji wa siku chache katika mpango wao.
Baada ya kugundua shida, walijikuta wakirudisha hatua zao na wakakimbia kando ya kijito hadi walipoona ukanda. Macho yao yaligundua safu ya vibanda vidogo vilivyopangwa kwa duara. Katikati kulikuwa na sangara inayotumika kupika wanyama wa porini. Kuta hizo zilijengwa kwa shina kubwa, la mianzi ambalo lilikuwa limefungwa pamoja na kufungwa na tope na nyasi zilizopasuliwa. Paa hizo zilitengenezwa kwa majani ya mitende yaliyofumwa pamoja. Kwenye ncha kulikuwa na shimo ambalo lilitumika kama mahali pa moto, ambalo lilifunikwa na muundo zaidi wa umbo la koni.
Kwa mshangao wao mkubwa waligundua kuwa kijiji kilikuwa karibu na eneo la kutua kuliko ilivyotarajiwa.
Baada ya kuona wageni, wakaazi wote walitoroka, wakijificha katika vibanda vyao. Walionekana karibu kama mipira ya mchezo wa pool inayopigwa na mpira wa kuanza mchezo.
Walijikuta mbele ya kabila moja la mwisho la Bonobo ambalo lilikuwa halijatawaliwa na Waaniki kwa kupata makazi katika eneo kama hilo lenye uhasama.
Wanne hao hawakufanikiwa, hata hivyo, kwenda bila kuonekana. Baada ya sekunde chache wapiganaji wenye silaha na mikuki walijitokeza mbele yao.
"Tunakuja kwa amani." akasema Xam kwa haraka.
"Tunataka pia amani." alisema mpiganaji aliyekuwa na kitambi kubwa, ambaye alionekana kama bosi.
"Kwa sababu hii, tunataka uondoke!"
"Hatutafuti shida. Lakini tunahitaji msaada wako. Oalif alizungumzia ujasiri wako. "
"Oalif alituacha miaka mingi iliyopita. Kwa nini umekuja hapa? "
"Tunatafuta nyumba ya watawa ya Nativ."
"Kwa nini?"
"Tuko kwenye ujumbe wa amani ambao unahusisha watu wote."
"Wengi wamekuja hapa kwa kisingizio cha amani, lakini basi waliishia kusababisha vita tu."
"Lakini kama unavyoona, sisi sio Waaniki. Mimi ni Xam wa Tetramir. Lazima umesikia kutuhusu...
"Xam kutoka Sayari ya Sita?"
Xam aliguna.
"Nenda ukamwite yule mwenye busara." aliamuru mpiganaji huyo mwenye kitambi.
Xam hakutarajia kumwona mwenzake wa zamani akitoka ndani ya kibanda. Akamwita kwa jina lake:
"Xeri! Nakuona! Nilidhani wamekuondoa. "
"Xam? Unafanya nini hapa, rafiki yangu? Upiganaji ndani yangu umekufa: Nimeona rafiki wengi sana wakifa.
"Nimefurahi kukuona." Alishangaa Xam, akamkumbatia rafiki yake wa zamani.
"Pia mimi. Nini kilikuleta hapa? Yuko wapi Oalif? "
"Kama angejua kuwa uko hapa tusingeweza kumuweka ndani ya chombo cha angani. "Tunatafuta nyumba ya watawa ya Nativ."
"Basi hautalazimika kwenda mbali sana. Angalia tu juu. Iko kwenye kisiwa kinachoelea. "
Tetramir aliangalia juu na kugundua kuwa juu ya vichwa vyao upanga mkubwa wa mwamba ulikuwa ukining'inia juu yao. Ncha ya upanga ilikuwa imefunikwa kwenye miti ambayo ingeweza kuiga mambo ya ndani ya kisiwa hicho.
"Tutafikaje huko?"
"Sio karibu kama inavyoonekana. Usipotoshwe. Hakuna mtu aliyewahi kuifikia. Wengi wamejaribu. "aliendelea kuzungumza Xeri. "Umbali kati yako na kisiwa hicho hautabadilika licha ya maili zote utakazotembea. Ni kana kwamba iko katika mwelekeo mwingine. Angalia kote. Haionyeshi vivuli vyovyote ardhini.
Hawakuwa na hata wakati wa kutazama nyuma chini: wakati sikia sauti kama ya nyoka. Walimwona Xeri akianguka chini. Xam alimkimbilia kumsaidia lakini alielewa kuwa alikuwa amechelewa.
"Kila mtu ajifiche." akapiga kelele.
"Kwa silaha." Alifoka kamanda mpiganaji.
Watu walikuwa wametawanyika tena kote kama mipira ya pool, lakini wakati huu walikuwa wakitafuta makazi katika mashimo waliyochimba kwenye msitu.
Vita vilikuwa vikiendelea. Wanajeshi wa Mastigo walikuwa wamewafikia mapema kuliko ilivyotarajiwa. Watoto wengine walikaa katikati ya kijiji, wakigandishwa na woga.
"Tunapaswa kufanya kitu." alisema Xam lakini hakuwa na hata wakati wa kumaliza sentensi yake kwamba smpiganaji wa Oria alikuwa tayari ameporomoka kuwalinda na ngao yake.
Xam alimfunika kwa kuchoma eneo lililowazingira, wakati Ulica, ambaye alikuwa amepanda haraka juu ya mti, shukrani kwa mabawa yake ya kijivu, alianguka kimya kwa askari wa Mastigo, ambao walikuwa wamejificha vichakani. Na yeye akawapiga hadi kufa, kama Kipanga inavyopiga mawindo yake.
Mara tu baada ya hapo, wanawake walikimbia kwenda kuwakamata watoto wao ambao walikuwa wamekingwa na mwili wa Zàira, ambaye alikuwa amelala chini amejeruhiwa. Xam na Ulica walimkimbilia.
Mraba huo ulikuwa tupu, na upepo mkali ulianza kuvuma kama kimbunga kikiendelea katikati ya kijiji, lakini bila kuharibu njia yake. Zàira, Xam na Ulica walihisi miili yao yanakuwa migumu. Kama kwa uchawi, kuna kitu kilikuwa kikiwashika na kuwazuia kukimbia. Walizunguka kwa sekunde kadhaa kabla ya kutupwa kwenye ukingo wa kisiwa kinachoelea.
Kwa sekunde Ulica alihisi kana kwamba alikuwa akielea hewani. Kichwa chake kilikuwa bado kinazunguka kama wakati alikuwa mtoto na angecheza mchezo wa kujizungusha na rafiki zake. Haraka alipata fahamu na kwenda kuwatafuta wenzake.
Xam alikuwa tayari amempata Zàira, ambaye alikuwa amezimia na akapiga magoti karibu naye: macho yake meusi yalikuwa yamejaa huzuni na yalikuwa yakionesha udhaifu wake kwa yule msichana wa Orian ambaye alikuwa akiandamana naye kila wakati katika vituko vyake.
Ulica alitembea kuelekea kwao na akiwa na busara kama kawaida, alianza kumtazama Zàira. Aliangalia mapigo yake na kusema:
Mapigo yake ni ya chini, lakini hakuna kitu kibaya sana. Mwili wake unajaribu kupunguza nguvu, ili aweze kupona.
Aligeuka kwa uangalifu kutambua ni wapi alikuwa amejeruhiwa. Kwa upole akavua nguo isiyokuwa na sehemu mgongo hadi kiunoni kwake ambayo alikuwa ameifunga nyuma ya shingo yake na kumruhusu atembee kwa uhuru.
"Ana jeraha kwenye nyuma ya nyonga yake ya kushoto. Kwa bahati nzuri ni ndogo tu. Silaha hizo zilimlinda. "
Hakuwa amepoteza damu nyingi kwani miale ya lesa ilikuwa imejeruhi ngozi ya juu tu.
"Haionekani kama viungo muhimu viliharibiwa, la-sivyo angekuwa tayari amekufa." aliendelea Ulica.
Xam alikuwa akimwangalia kwa kushangaza. Mtu huyo ambaye hakuwa na utulivu kwamba wakati wa vita asingehisi hofu yoyote au huruma kwa maadui yake, mtu huyo ambaye alikuwa amezoea vitisho na damu ya uwanja wa vita, hakuweza kutamka neno.
Akaitikia kwa ishara ya idhini.
"Lazima tutafute mahali pa kutibu jeraha." alipendekeza Ulica.

Xam tayari alikuwa amemchukua Zàira na alikuwa akiendelea kuelekea kile kilichoonekana kama hekalu juu ya kilima kijani kibichi.
Ukaribu wake na harufu yake ilimkumbusha wakati huo wakati wa utoto wakati Zàira alimtoa nje ya Korongo ya fuwele huko Oria. Ilikuwa imetokea katika moja ya nyakati chache ambapo alikuwa ameacha chuo hicho, ambayo ilikuwa familia yake pekee anayoijuia.
Wakati wa likizo ya shule, rafiki zake wengi walikuwa wakirudi nyumbani kwa familia zao. Walakini, sio watoto wote walikuwa na bahati: wengine wao walikuwa yatima kama Xam, wengine wangebaki kwenye chuo hicho kwa sababu wazazi wao walikuwa na shughuli nyingi za kazi; wengine wangerejea kwa familia ambazo zilikuwa na kazi nyingi. Kawaida kambi ya majira ya joto ilipangwa na mara nyingi mahali pa kwenda ilikuwa Oria.
Kwenye sayari hiyo, hewa ilikuwa nadra kwa sababu ya vipimo vyake vidogo ambavyo vilisababisha nguvu ndogo ya mvuto. Wale wote ambao hawakutoka Oria ilibidi wabebe kifaa cha kuongeza hewa ili kuhakikisha oksijeni bora. Bila hiyo, wangehisi kukosa pumzi kana kwamba wako juu ya mlima.
Kambi ya msimu wa joto huko Oria ilidhihirishwa kwa safu ya majukumu, lakini mwisho wa shughuli za kila siku, Xam angejikuta akisababisha shida katika eneo la chuo hicho. Karibu na hapo kulikuwa na shamba: lilikuwa la baba ya Zàira na ndivyo alivyokutana naye.
Wakati huo wa joto urafiki wao ulizidi kuwa na nguvu. Kama vijana wote, walipenda kuingia katika shida kubwa zaidi. Usiku huo Zàira, kwa kweli, alimwambia Xam kuhusu mahali anafikiria kuna uchawi. Walakini, aliweka sherehe ya hadithi hiyo kwa siri ili asiharibu mshangao, lakini zaidi ya yote, hakusema kuwa watu wazima watakataza kwenda huko kwa sababu ya hatari zake.
Ndio jinsi alivyomvuta rafiki yake katika safari yao ya jangwani. Alimwuliza Xam avae buti zake nene na akamkataza kuleta rafiki yeyote: itakuwa ziara yao.
Walitembea kwa muda mrefu na Xam hakuweza kuelewa Zàira alikuwa amemfanya avae buti hizo mbaya katika siku hiyo yenye joto kali.
Zàira hakuwa mtu wa kuzungumza sana, kwa hivyo walitembea kwa muda mrefu wakiwa kimya hadi Xam, ambaye alikuwa amechoka, aliuliza:
"Ni maili ngapi kabla ya kufika huko?"
"Usiwe mdhaifu. Tuko karibu kufika. "alijibu Zàira.
"Natumai ni ya muhimu!"
"Ndio, usipoteze imani. Tunachohitaji kufanya ni kupanda juu ya mlima ule. "
"Wacha tuone ni nani anafika hapo kwanza." alipiga kelele Xam wakati alipoanza kukimbia.
Zàira alimfukuza, akijaribu kumzuia kwa vyovyote vile, lakini Xam, ambaye sasa alikuwa kasi, hakusikia akija.
Aliweza kumkabili juu ya milima.
Xam, ambaye alikuwa amelala kifudifudi na kushangaa, akamgeukia:
"Kwanini alinirukia?"
"Je! Umegundua chochote?" alisema Zàira, akiashiria kitu juu ya milima kwa kidole chake. "Je! Ulitaka kuingia ndani?"
"Wow, ulikuwa sahihi. Inashangaza! "
Mazingira ya kupendeza yalikuwa yakionekana mbele ya macho ya Xam: korongo kubwa mbele yao.
Haikuwa pana sana, lakini waliweza kuona chini hata hivyo. Pande hizo zilikuwa zimepambwa kwa mlalo wa vivuli vilivyongaa. Rangi ilikuwa zuri na dhahabu karibu na ncha ya korongo, ilihali ilikuwa nyekundu zaidi karibu na chini. Iligawanywa katika sehemu mbili: ile ya kwanza, ambayo ilikuwa mbali zaidi kutoka kwao, ilifunikwa na fuwele za amethisto ambazo zingeonesha rangi ya mwamba. Ya pili ilikuwa imejaa maua makubwa, yenye umbo la kengele ambayo watu wawili wangeweza kukaa chini yake. Umbo huo wa Kengele ulikuwa ukisonga bila kusimama. Kwa njia hii ungeruhusu mmea kuhifadhi oksijeni zaidi na kuonesha mandhari ya kupendeza.
Kwa kushangaza, Xam alihisi kuwa mwili wake ulikuwa mwepesi kuliko kawaida. Alikuwa akiangalia huku na kule akishangaa, na matembezi hayo yote yalimfanya ahisi njaa.
"Sawa, hapa ni mahali pazuri pa vitafunio. Natumai kwamba umeleta chakula kwenye mkoba wako. "
"Daima unafikiria kuhusu chakula." alitabasamu Zàira.
Akatoa kamba kwenye mkoba wake. Alivua buti na kuifunga kwenye kichaka. Baada ya hapo alikaribia korongo.
Xam hakutambua rafiki yake alikuwa akifanya nini.
Hakuwa na hata wakati wa kuuliza kabla ya kumwona Zàira akiruka kwenye eneo tupu. Hofu iliwashinda kabisa na kukimbia kuelekea pembeni kuona ni wapi alikuwa ameenda.
Alitazama pembeni na kumuona Zàira akicheka na kuelea hewani.
Kwa wakati huo angetaka kumuua akizingatia jinsi alivyokuwa amemwogopesha, lakini wakati huo huo alihisi kufarijika na kufurahi kumwona.
Zàira haraka alielea kuelekea ukingoni na kutua karibu na Xam.
"Wewe ni mwendawazimu? Nilidhani umegonga miamba! Ungeweza kunionya! " alisema akiwa na hasira.
"Na kukosa uso wako? Ungepaswa kuijiona mwenyewe. "alisema akicheka sana.
"Umefanya vizuri!" alijibu kwa kejeli Xam, ambaye alihisi kutaniwa.
"Samahani, sikukusudia kukutisha." aliongeza Zàira akigundua kuwa labda alikuwa amekwenda juu.
"Usijali. Badala yake, unafanya nini na vifaa hivi vya hewa? "
Aliuliza Xam akiwa na tabasamu kubwa usoni mwake kwani alikuwa anafikiria kuwa hangeweza kushikilia kinyongo naye.
Vilikuwa vifaa vya kawaida ambavyo vilitumika sana kwenye Oria kusafisha kifaa cha kupoza injini za matrekta ambazo zimejaa mchanga.
"Wanatoa msukumo wa mwisho kwamba ninahitaji kurudi ndani. Hewa iliyoshinikizwa ilinisaidia kushika kazi na kuweza kuzidi ongezeko dogo la mvuto kwenye mpaka. "
"Unaendeleaje?"
"Inashangaza ..."
"Huamini! Usitie wasi wasi. "
"Sawa. Kwa kweli, papo hapo kwenye kituo hiki mchanganyiko kati ya mvuto wa chini na msukumo wa kwenda juu ulioundwa na maua makubwa ndio unaoturuhusu kuruka. Njoo. Vua viatu na unifuate. "
"Wewe ni mwendawazimu?" akasema, lakini alijua kwamba hatapinga.
"Kaa mbali na fuwele." "Huogopi, sivyo?" alimtania Zàira.
Xam alikaa pembeni, akavua buti zake na kuzifunga pamoja na ile ya Zàira. Moja kwa moja baada ya hapo aligundua kuwa walikuwa wakielea hewani na bila buti alikuwa akihisi mwepesi zaidi. Hakuweza kuweka miguu yake chini.
"Weka hii mfukoni." alisema Orian huku akitoa nje ya mkoba wake vifaa viwili. "Mara ya kwanza turukaa kwa pamoja."
Walitembea wakiwa wameshikana mkono hadi pembeni na kuruka ndani ya utupu bila kusita, kama vijana tu wanavyoweza.
Waliruka pamoja kwa muda hadi Xam alipokuwa hana wasi wasi tena. Ndipo Zàira akafichua mshangao mwingine.
Aliburuza Xam kupitia kwa moja ya maua, ambayo yaliwafyonza ndani. Walianguka kwenye zulia laini yenye sulubu ya harufu nzuri. Maua hayo, ambayo yalikuwa ya samawati kwa nje, kwa ndani yalikuwa ya manjano au ya rangi ya waridi na sulubu kubwa ya machungwa. Xam hakuwa na hata muda wa kushangaa kwamba wote wawili walitupwa nje ya ua hilo. Rafiki hao wawili walianza kucheka bila kukoma.
Zàira alijaribu kuelezea, kati ya kicheko, kwamba ndani ya maua yatatoa kioevu cha kucheka.
Wakati huo, Xam alikuwa tayari kuruka peke yake na akamwachia Zàira, ambaye hadi wakati uliopita alikuwa amemshikilia kwa nguvu.
Raha hiyo ilikuwa imeshika kasi na Xam aliendelea kuingia na kutoka ndani ya maua.
Zàira alijaribu kukaribia: alikuwa amesahau kutumia kioevu cha kucheka kupita kiasi kwani kingeishia kumfanya apoteze mawasiliano na ukweli.
Haikuchukua muda mrefu kabla jambo hilo kutokea. Xam alikuwa amepoteza akili na alikuwa akikaribia hatari karibu kwenye eneo lililokatazwa.
Zàira alifikiri ilibidi aingilie kati kabla ya kuchelewa: glasi kali ingemwua. Xam, hata hivyo, alikuwa akienda kwa kasi sawa na yeye. Kwa hivyo, isingewezekana kumfikia. Alitoa mifukoni mwake vifaa vyake vya hewa na kutumia kwenda haraka. Alimfikia rafiki yake, ambaye alikuwa akicheka na alikuwa hajatambua kuhusu hatari iliyokuwa karibu na akamburuta mbali sekunde chache kabla ya kugonga ukuta.
Alimbeba kutoka kwa maua na hakumwachilia mpaka walipokuwa chini. Mara tu walipofikia kwenye chombo sahihi, alimfanya arudishe vifaa vya hewa. Alimshika kwa nguvu mikononi mwake wakati alikuwa akimzuia kwenye ukingo wa korongo.
Walijua kwamba walikuwa karibu kuhatarisha maisha yao wenyewe, lakini hawakuweza kuacha kucheka. Walilala chini, bega kwa bega, upande kwa upande, na kwa furaha walingojea athari ya maji ya kicheko kuisha kabla ya kurudi nyumbani.
Sura ya Tatu

Mikunjo kwenye ngozi yake ilikuwa ukifunua macho na kinywa cha kiumbe hicho

Sasa ni Zàira ambaye alikuwa katika hatari na umbali kati yao na kilele cha mlima ulionekana kuwa hauna mwisho. Kuba mweupe ulionekana wazi wazi. Ilionekana kama mzinga wa nyuki uliofunikwa kwenye vioo vyenye sita na ambavyo vinaonyesha mwangaza wa jua.
Kadri walivyokuwa wakikaribia monestari, ndivyo walivyokuwa wanahisi amani zaidi ndani ya mioyo yao.
Xam, ambaye alikuwa amechoka kabisa na uzito wa rafiki yake, aliendelea kutembea hadi walijikuta mbele ya upinde ulioelekea ndani ya hekalu.
Mara tu walipoingia ndani, mwili wa Zàira ulianza kuelea mbali na mikono ya Xam, ambaye hakupinga nguvu hiyo kwani alijua hakuna hatari.
Alikuwa akibebwa kuelekea korido ndefu hadi alipotoweka.
Mamia ya nguzo nyembamba yalikuwa yakishikilia chumba kikubwa cha uwazi ambacho kilikuwa kikiangalia Ulimwengu wote, kana kwamba utawa ulikuwa ukielea angani. Ulica na Xam waligundua kiumbe mwenye umbo la kushangaza nyuma ya barabara.
Mwili wa silinda, kijivu-zambarau ulijumuisha kichwa na sehemu nyingine nne, kila moja ikiwa na miguu miwili. Kilichoonekana kama pua kiliumbwa kama tarumbeta na kilichukua angalau nusu ya uso. Ilionekana kama kitu au mtu alikuwa ameisukuma nje. Mwishowe, mikunji kwenye ngozi yake ilikuwa ikifunua macho na mdomo wa yule kiumbe. Mwili haukuwa mrefu kuliko begi lililojaa unga.
"Ninaweza kuhisi nguvu chanya. Samahani kwa kukuvuta hapa, lakini kile mwenzako alifanya kilinishangaza. "
"Kwamba mwenzetu hakutushangaza. Tunafahamu ukarimu wake. Hatupaswi kuhusika na wale viumbe wasio na hatia. Tumepoteza muda mwingi kuzurura msituni, ambayo iliruhusu Mastigo kutambua tunakoelekea. Kwa hivyo, aliwaongoza walinzi wake kwa mahali penye upole na amani. Kosa kama hilo lisilosameheka kwetu. "alielezea Ulica.
"Isingewezekana kwa Tetramiri kufika mbali bila kuwaburuza viumbe hao maskini kwenye vita."
"Unajuaje sisi ni nani?"
Alijaribu kumwuliza Ulica, lakini Xam alimzuia ghafla wakati yeye mwenyewe akimfikia mkono wake:
"Zàira yuko wapi?" aliuliza kwa mtawa, ingawa aliweza kuhisi kuwa hakuna jambo baya lililokuwa likimtokea rafiki yake mahali hapo.
"Usijali. Yuko salama. Anaendelea kupata nafuu. Atakutana nasi hivi karibuni. "
Jibu hilo halikuwa dhahiri, lakini bado aliweza kuhisi hisia hiyo ya amani na ustawi.
"Unajuaje sisi ni nani?" aliuliza tena Ulica, ambaye alitaka kuelewa ni nani wanashughulika naye.
"Naitwa Rimei." alitamka yule kiumbe, bila hata kushughulikia swali la msichana huyo. "Niko hapa kwa mafungo ya kutafakari. Nafsi na matendo yenu, hata uzuri wa Eumenide ambaye sikumbuki jina lake. "Ilionekana kana kwamba ilikuwa ikifurahia kuridhika na uovu wake." Wamevutiwa kwangu, hata baada ya miaka 300. "
"Ulica." uso wake mzuri na maridadi haukuvutiwa na pongezi hiyo.
Alikuwa mwembamba na mdogo na alijua sura yake na hakuificha. Kabila la mtu huyo halikuegemea kuchumbiana, lakini hawangeficha maoni na hisia zao. Wangeweza kuzaa kama vipepeo kwenye kifukofuko kilichobeba rangi ya mtoto ambaye hajazaliwa. Wana-eumenide walikuwa na rangi tofauti, wote walikuwa na rangi wa aina aina.
Ulica alikuwa mmoja wa vizazi vya hivi maajuzi: wote waliumbwa kwa vinasaba. Katika sayari tukio lisilo la kawaida wakati wa vita kubwa vya mwisho lilikuwa limesababisha mabadiliko katika mhimili wa sayari ambayo ilisababisha kubadilika kwa mazingira na sumaku, na kusababisha kutoweka kwa idadi ya wanaume. Hata mtaalam wa jiolojia ulimwenguni hakuweza kupata sababu ya tukio hilo.
Ili kuzuia kutoweka kwa spishi nzima, Wana-eumenide waliamua kuongeza mbolea ya vitro ya jeni ya viumbe vya kiume zitumike kama mbolea isiyo asili.
Wangeweza kuunda viinitete tu vya kike ili kuzuia wanaume wengine kuzaliwa na kwa hivyo kufa. Hawakuwa tayari kukubali kushindwa. Walikuwa wakitafuta katika DNA yao kwa jeni ile ile ambayo iliwaruhusu kuishi na kuipandikiza kwenye DNA ya kiume. Kwa njia hii haingeweza kuathiriwa na hali mpya za mazingira.
"Bado hujaniambia imekuwaje ujue sisi ni nani." alisisitiza Ulica.
"Kwa sababu naona vitu vingi. Nimekuwa nikisubiri maswali yako kwa muda mrefu. "
"Maswali gani?" aliuliza Xam, ambaye alionekana kuchanganyikiwa wakati alikuwa akipapasa ndevu zake nene, nyeusi, zilizojikunja.
"Maswali yako kuhusu Kirvir." alimtarajia Ulica. "Ulikuwa unazungumza nini hapo awali?" aliuliza kwa mtawa. "Je! Unataka kuona nini?"
"Ninaweza kuona yote yanayotokea kwenye sayari, lakini kwa bahati mbaya wakati mwingine habari hukaa ndani yangu kwa muda mfupi.
"Fafanua fupi."
"Inategemea. Wakati mwingine hukaa milele, wengine hupotea baada ya siku au saa kadhaa. "
"Unaweza kutuambia nini kuhusu Kirvir?" aliuliza Xam.
"Kirvir ni kila kitu: inatuzunguka, inatuweka pamoja na kututenga. Ikichochewa, inageuka kuwa kitu kingine. Inaonekana inaweza kutawaliwa lakini ukweli ni kwamba inatoroka. Inaweza kuwa ya busara au hatari sana. "
"Hausemi chochote kipya kwetu." alitoa maoni Ulica.
"Hakuna jipya ya kujua. Kila kitu tayari kinatuzunguka. "alijibu yule mtawa. "Unachotakiwa kufanya ni kuiruhusu ikuchukue katika njia inayofaa."
"Ikiwa kweli unaweza kuona kila kitu, basi tayari unajua lengo letu. Tusaidie kuidhibiti. "Ingeweza kurejesha mzawazo." alisema Xam.
"Ni dhahiri kwamba inataka kusaidia." alisisitiza Ulica. "Au isingetuongoza hapa. Suala hapa ni jinsi. "
"Usiwe na haraka, mpendwa. Nimesubiri kwa muda mrefu sana kwa muda huu. Imepita miaka mia tatu tangu niongee na mtu. Usiondoe fadhila hii kwangu. Saa ni kipimo kwa viumbe vyote ambavyo sio vya Kirvir. Baada ya yote, nilifikiria sana hii. "
"Lakini tunaishi wakati wetu na tuna jukumu kwa wale kama sisi. Vita vinakuja. "alidai Xam.
"Utakaa hapa kwa muda mrefu kama ni lazima, ikiwa unataka majibu ya maswali yako. Sio juu yangu. Itakuwa Kirvir kutathmini ni muda gani unahitaji kukuonesha njia. "

Baada ya dakika chache, au angalau ndivyo Tetramir alihisi, walimwona Zàira akitokea kwenye korido ndefu, iliyoangazwa.
Xam haraka alimwendea, akijaribu kuficha hisia zake.
"Unahisije?" alimwuliza.
"Nini kilichotokea?" aliuliza Zàira.
"Umeumizwa. Je! Hukumbuki? " alisema Xam, akimpa mkono wake ili kumsaidia.
"Mimi niko sawa. Usijali. "alimhakikishia Orian, akikubali msaada wake. "Ndio, nakumbuka. Lakini tuko wapi? "
"Tuko ndani ya monasteri. Kwenye kisiwa kinachoelea. "
"Tumeamkaje hapa?"
"Ishara yako ilimvutia yule mtawa, ambaye alituleta hapa kwa kimbunga."
"Halafu, Xam alikuchukua hadi kwenye nyumba ya watawa." aliongeza Ulica.
"Asante." alijibu Zàira akimtazama Xam moja kwa moja machoni, ambaye kwa wasiwasi alitazama pembeni. "Inaonekana kama imekuwa miezi kadhaa tangu nilipigwa risasi mgongoni."
"Ni kweli." aliingilia kwa ujasiri Rimei. "Ulitengenezwa na kuponywa katika chumba cha wakati ili tuweze kuharakisha mchakato wa uponyaji. Utahisi tu umekuwa kwa miezi michache kuliko vile ulivyokuwa. "
"Asante." alisema Zàira, ambaye siku zote alikuwa mwanamke wa maneno machache.
Ulica akaanza kuongea:
"Tuambie zaidi kuhusu Kirvir, yaani nishati ambayo husababishwa wakati wa usawa wa sayari. Tunaweza kuiweka mikononi mwetu ili kuepuka vita vya ukombozi wakati wa usawa.
"Kusimamia Kirvir sio rahisi. Lakini kabla ya kuzungumza kuhusu hayo, lazima niongee na wewe kuhusu wajumbe." mtawa akaanza kuongea. "Wajuzi ambao walikuwa wakitafuta amani kama wewe." Walikusanyika hapa kuelewa utendaji wake. Kila mmoja wao alijua siri fulani na kwa kujiunga na vikosi vyao, waliweza kujenga upya tabia ya mambo yote hayo ambayo Kirvir huibuka. Nao walifanya hivyo kwa kuyaandika kwenye ngozi. "
Kwa hivyo Xam, ambaye alishangaa, aliuliza:
"Kwa hivyo, ngozi hiyo haina nguvu yoyote ya uchawi?"
"Kwa usahihi" aliendelea Rimei. "Lakini ni muhimu kujua jinsi ya kuongoza Kirvir na kiumbe kinachoweza kuitumia. Imekuwepo tangu mwanzo wa wakati. Kiini chake ni laini na bila kujua. Hakuna kinachoweza kuiharibu. Inaweza kuyeyuka na kuzaliwa upya na huwa inategemea mlinzi. Inajulikana kama Tersal. Zaidi ya hayo, kuna vitu vingine sita ambavyo kiumbe hicho kinaweza kuingiliana. Sababu ambayo Kirvir ina nguvu sana wakati wa usawa wa sayari ni kwa sababu ya ukaribu wake wa vitu vyote kwa Tersal.
Wajuzi walianza harakati zao za vitu hivi. Wakajikuta kwenye sayari sita za mfumo wa jua. Mara tu baada ya kuzifuatilia, wajuzi walijaribu kutekeleza yale waliyoandika kwenye ngozi, lakini walizuiliwa na moja ya vita vya usawa wa sayari wakati huo. Kwa hivyo, baada ya kugundua kuwa kuungana tena haitawezekana, kila mmoja wao alificha kitu chake katika sayari yake mwenyewe ili isiangukie mikononi mwa adui. Kama unavyojua, sayari nyingine au hata zote za mfumo wetu wa jua, wakati wa kukamilisha mizunguko yao, zinaweza kuishia kwa mstari sawa. Hii inasababisha usawa wa sehemu au jumla. Kadiri sayari zinavyohusika, ndivyo ushawishi wa Kirvir unavyokuwa na nguvu, na kuifanya miili yao kuwa ya ajabu zaidi na kutia nguvu athari kwa utulivu wa kihemko wa wenyeji. Ni wazi kwamba, kutakuwa na kilele wakati wa mpangilio kamili. Ukaribu na sayari zilizounganishwa na matukio haya zimechochea roho na kusababisha vita vya kikabila. Kadri muda ulivyokuwa ukipita, uadilifu wa watu wengi ulikuwa umekua kwa kuunda maoni ya amani, utulivu na haki ya kila kabila kukua kulingana na mila na desturi zao. Hiyo iliwezesha kuundwa kwa Muungano ambao mnawakilisha. Carimea na Medusa tu ndio wameamua kujitenga nayo: ya kwanza inakaliwa na wanyama wa kuwinda, ya pili kwa sababu inaongozwa na kabila lenye uchoyo ambayo imeanzisha ustawi wake kwa damu na unyanyasaji.
"Ngozi iko wapi?" aliuliza Ulica.
"Sijui iko wapi. Lakini naweza kusema ni nani alikuwa wa mwisho kumiliki hiyo. Jina lake ni Wof. "
"Wof, shujaa wa Sayari ya Sita?" aliuliza Xam.
"Ndio."
"Je! Unamfahamu wewe mwenyewe?" aliuliza Ulica kwa Xam.
"Alikuwa nahodha wangu wakati nilianza kupigana dhidi ya serikali. Alikamatwa wakati wa moja ya vita maarufu zaidi. Aliweza kuweka mikakati ya kuzuia Aniki na wanajeshi kadhaa tu. Hii iliruhusu wanajeshi wetu kupewa majukumu mapya na kushinda vita ambavyo tayari vilionekana kutoshindwa. "
"Kutoka kwa habari yetu ya mwisho tunajua kwamba ameshikiliwa kwenye Mwezi wa Enas." alisema Ulica. "Tunatumai bado yuko hapa. Ruegra anahakikisha anahamishwa kila baada ya muda, ili kumzuia kuachiliwa. Yeye ni mmoja wa maadui wake mbaya zaidi. "
"Kumwachilia sio rahisi." alitoa maoni Zàira.
"Unaweza kutuambia nini kuhusu kiumbe hicho?" aliuliza Ulica.
"Sijui Tersal iko wapi. Itajifunua kwako wakati wa ukaaji wako kwenye kisiwa maadamu mioyo yako ni safi. Lakini naweza kukupa habari zaidi kuhusu vitu hivyo. Ni vitu vya kila siku. Ndani ya kila mmoja wao kuna vito. Vito hivi vinatoka kwa jiwe moja kubwa ambalo lilikuwa likiwakilisha Kirvir kwa nguvu zake zote. Vito hivyo viligawanywa mwanzoni mwa nyakati ili kuepusha kwamba nguvu hizo nyingi zinaweza kuanguka mikononi mwa mtu mmoja. Kila moja ya vitu hivi iliabudiwa kwa muda mrefu. Utafiti kuhusu nguvu zao halisi, hata hivyo, haukufanywa kwa kina kwani zingebadilika au hata kutoweka kulingana na ukaribu au umbali kati ya sayari, na kusahauliwa kwa muda. Kwa hivyo, walitunzwa na wale ambao walikuwa wamejitolea kwao.
"Je! Huwezi kutupa chochote sahihi zaidi?" aliuliza Ulica.
"Ni jioni tayari. Ni bora ikiwa sote tutapumzika. Fuata taa, zitakuonesha njia ya vyumba vyenu vya kulala. "
Nuru tatu za mwangaza zilionekana kutoka juu ya mikono yake ya juu na kujiweka mbele ya kila mmoja wao.
Rafiki hao watatu waliongozwa kwa vyumba tofauti. Zilikuwa seli za watawa. Kuta zilikuwa zimepakwa rangi nyeupe na zilikuwa na kitanda tu na dawati ndogo la kuandikia. Juu ya dari iliyopinda, dirisha lenye pembe sita lilikuwa linaleta nuru ndani ya chumba.
Ulica alikaa kwenye dawati na kutoa tarakilishi yake kwenye mkono wake. Akaiwasha na kuiweka juu ya dawati. Kibodi ilionekana juu ya dawati na skrini kwenye ukuta. Alianza utafiti wake.
Xam alijitumbukiza kitandani na akalala mara moja kwani alikuwa amechoka, wakati Zàira alisali kabla ya kwenda kulala.

Конец ознакомительного фрагмента.
Текст предоставлен ООО «ЛитРес».
Прочитайте эту книгу целиком, купив полную легальную версию (https://www.litres.ru/pages/biblio_book/?art=65495147) на ЛитРес.
Безопасно оплатить книгу можно банковской картой Visa, MasterCard, Maestro, со счета мобильного телефона, с платежного терминала, в салоне МТС или Связной, через PayPal, WebMoney, Яндекс.Деньги, QIWI Кошелек, бонусными картами или другим удобным Вам способом.